Tuesday, October 29, 2013

KINANA AZIMA MAPINDUZI



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alilazimika kuzima mapinduzi yaliyokuwa yamepangwa kuwang’oa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana ya chama hicho (UVCCM), Sadifa Juma Khamis na makamu wake, Mboni Muhita.

Jana Kinana akifungua mkutano wa Baraza Kuu la jumuiya hiyo, aliweka bayana kuwa mkutano huo haukuwa kwa ajili ya “kuibomoa UVCCM, bali kuijenga”, kauli ambayo inatajwa kuwa iliwavunja nguvu wajumbe waliokuwa wamepanga kuanzisha harakati za kuwatoa madarakani viongozi hao.

Habari zaidi kutoka Dodoma zilisema kauli ya Kinana iliongeza nguvu harakati za kujinasua za Sadifa ambaye usiku wa kuamkia jana, alikesha akifanya vikao vya kuwaomba radhi wenyeviti wa UVCCM wa mikoa na baadaye wajumbe wote wa Baraza Kuu.

“Hatua hiyo nadhani imemsaidia sana maana wenzake ndani ya umoja huo hawaridhiki na jinsi mambo yanavyokwenda, pamoja na uongozi wake. Wanaona kama hakidhi standards (viwango) zao,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya mkutano huo.

MWANAFUNZI AJIUA KUONDOKA NA AIBU

MWANAFUNZI wa Darasa la tano Katika Shule ya Msingi Kitanda katika halmashauri ya wilaya ya Tunduru aliyefahamika kwa jina la Faudhia Suleiman Ally Kawalula (14) amejinyonga hadi kufa kwa madai ya kuondokana na aibu ya tukio la Wizi.

Mashuhuda wa Tukio hilo walisema kuwa Mwanafunzi huyo alikutwa akiwa aejinyoga kwa kutumia kamba asubuhi ya kuamkia oktoba 27 mwaka huu nda ya chumba alicho kuwa akilala nyumbani kwao.

Wakizungumzia chanzo cha tukio hilo kwa masharti ya kutotajwa majina yao gazetini miongoni mwa mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa kabla ya mwanafunzi huyo kuchukua maamuzi hayo alituhumiwa kuiba Tsh. 5000 kwa muuza duka jirani na nyumba yao .

Walisema baada ya tukio hilo ambalo lilidaiwa kufanyika kwa ustadi mkubwa na alipo guindulia tayali akuwa amekwisha nunua nguo za ndani, mafuta ya kupaka na sabuni vitu ambavyo muuza duka huyo alivitaka
apewe ili aviuze kwa ajili ya kufidia fedha yake hali ambayo ilimuweka binti huyo katika aibu na kumfanya achukue hatua hiyo.

Monday, October 28, 2013

VIONGOZI CHADEMA WAZIPIGA KAVUKAVU

Mkutano wa Baraza la Uongozi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini juzi uligeuka ukumbi wa ngumi, baada ya Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba kushushiwa kipigo.

Mwigamba alishushiwa kipigo hicho na baadhi ya viongozi wenzake wa chama kwa madai ya usaliti na tayari amesimamishwa uongozi kwa muda usiojulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas jana alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na viongozi hao wa Chadema kufikishana polisi.

Alikutwa na zahama hiyo mbele ya viongozi wakuu wa Chadema Taifa, Mwenyekiti, Freeman Mbowe na mwasisi wa chama hicho, Edwin Mtei katika Hoteli ya Coridal Spring.

Saturday, October 19, 2013

TLC KUZINDUA FILAMU

Kundi la TLC linatalajia kufanya uzinduzi ya filamu yao mpya inayojulikana kwa jina la CrazySexyCool.

TLC inatarajia kuizindua filamu hiyo wiki ijayo ambapo teyari wameshaanza kuonesha baadhi ya vipande vya filamu hiyo.

MECHI YA YANGA NA SIMBA ULINZI WAIMARISHWA

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama vimejipanga ipasavyo kuakikisha Ulinzi unakuwepo Uwanja wa Taifa  wakati wa mchezo wa watani wa jadi kati ya Simba na Yanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam jana,Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Kamishina Suleiman Kova alisema  mchezo wa leo utakuwa na mvuto mkubwa kwa mashabiki wa Tanzania na wale wa nchi za Afrika Mashariki tutokana na hali hiyo jeshi la Polisi limejipanga kupambana na hali yoyote ya uvunjifu wa amani itakayo jitokeza katika mchezo huo.

"Tunaomba wananchi wasiwe na shaka yeyote ya kiusalama na pia watupe ushirikiano wa kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi kwa jambo lolote wanaloisi linaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa ndani ya uwanja au nje."alisema Kova.

Wednesday, October 16, 2013

WAZEE YANGA YAJITAMBA KUINGO'A SIMBA

WAZEE wa Club ya Yanga wametamba kuwafunga watani wao wa jadi Simba katika mechi yao ya kesho kutwa inayotarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambapo wamedai kuwa mnyama lazima afe.

Akizungumza kwa niaba ya wazee hao na Waandishi wa Habari Dar es Salaam Katibu wa Baraza la Wazee Ibrahim Akilimali alidai kuwa  timu hiyo ndiyo inaanza kucheza mchezo wao wa ligi rasmi huku wakijitapa kumuua mnyama kutokana na maandalizi yao ambapo kikosi cha Yanga kitapanda dimbani huku kukiwa hakuna majeruhi.

Friday, October 4, 2013

SERIKALI KUBORESHA ELIMU NCHINI

SERIKALI inatakiwa kuboresha kwanza maslahi ya walimu na vifaa mashuleni ili kupatikane na matokeo makubwa (Big Result Now)

Hayo alisema Mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika wakati akikabidhi madawati 120 yenye thamani ya shmilioni 12 katika shule zilizoko Kata ya Manzese ambao walikuwa na uhaba wa madawati na kusababisha wanafunzi kukaa chini .

Alisema kuwa walimu wamekuwa wakililia maslahi yao kila siku lakini serikali haiwasikilizi hivyo itasababisha matokeo mabya ya mitihani kila siku.

COKE STUDIO YAZINDULIWA AFRIKA

KIPINDI cha muziki kinachojulikana kwa jina la Coke  studio Afrika chazinduliwa rasmi jana huku kikiwa na lengo la kuuboresha muziki wa Afrika uwe wa kisasa na unaolenga vijana.

Akizungumza katika uzinduzi huo Meneja bidhaa wa Coca Cola Tanzania, Maurice Njowoka aliweka wazi kuwa studio hiyo inathamini nguvu ya muziki katika kuwaleta watu pamoja bila kujali jinsia, lugha, dini na nchi.

Alisema kuwa kipindi hicho cha runinga kinachojumuisha nchi za Afrika Mashariki, kati na Magharibi kitawahusisha wanamuziki wa miondoko ya aina tofauti tofauti kutoka sehemu mbalimbali ili kupata mchanyato wa kisasa wenye asili ya Afrika.

Tuesday, October 1, 2013

WANAWAKE WAANDAMANA

NCHI ya Nigeria inakumbwa na uhaba wa wanaume wanaohitaji kuoa hali iliyosababisha wanawake zaidi ya elfu nane kuandamana.

Lengo la maandamano yao ni kushinikiza serikali kuwasaidia waolewe kutokana na uhaba wa wanaume hao uliojitokeza nchini humo.

Maandamano hayo yaliyofanyika nchini humo yalikuwa na nia ya kutatua tatizo hilo ingawa haikuweka wazi ni njia gani zitakazotumika kutatua uhaba huo wa wanaume.

Wanawake wengi walijitokeza katika maandamano hayo ambapo jumla ya wanawake 5380 waliopewa talaka, 2200 wajane, 1200 yatima, na 80 wengine kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.

Wanawake hao walidai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku hali inayopelekea kuhitaji kuolewa ili waweze kupata msaada kutoka kwa wanaume hao.

MAHALI YA WANAWAKE INAONGEZA UKATILI

IMEELEZWA kuwa  ukatili dhidi ya wanawake  katika ndoa unatokana na  kigezo cha
kulipiwa mahali ambayo imekuwa ikigeuka  kuwa ni adhabu  na chanzo cha mateso.

Hali hiyo imebainika kuwa  haitoi usawa  ndani ya jamii  kwani  mwanaume anaonekana yupo  juu na mwanamke kuwa chini  kutokana na wanaume kuwaona wanawake ni  mali yao Hayo yalielezwa jana na mwezeshaji  Fortunata Makafu  wakati akizungumza kwenye mafunzo ya siku mbili wilayani Chamwino yaliyoandaliwa na Wowap kwa kushirikiana na shirika la Tunaweza na oxfam kwa viongozi mbalimbali wa kiserikali, dini, watmaalufu, polisi na watendaji wa kata na vijiji.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa shirika hilo limekuwa likitoa elimu kwa jamii ilkuepuka ukatili huo  na mafanikio mbalimbali yamenza kuzaa matunda.Alisema kuwa hivi sasa  kuna unafuu mkubwa  katika  kushughulikia  ukatili wkijinsia  kutokana na jeshi hilo  kuweka dawati la jinsia.

MTOTO WA MIAKA MIWILI AJIFUNGUA

MTOTO wa miaka miwili wa nchini China, amejifungua baada ya madktari kugundua kuwa anamimba isiyokuwa.

Mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Xiao Feng alijifungua kwa njia ya upasuaji mara baada ya madkati hao kugundua kuwa anaujauzito huo usiokuwa.

Xiao alipelekwa hospitali mara baada ya tumbo lake kuwa kubwa hali ambayo ilimsababishia matatizo ya upumuaji ndipo madktari walipoamua kumfanyia uchunguzi.

MSHITAKIWA AACHIWA HURU KWA FAINI YA 1000

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemlipisha faini ya Sh.1000 raia wa Kenya Joshua Mulundi baada ya kumtia hatiani katika kesi ya kuidanganya polisi kuhusika kumteka Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka iliyokuwa ikimkabili.

Shauri hilo jana lililetwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Aloyce Katemana, kwa ajili ya mshtakiwa huyo kusomewa maelezo ya awali ambapo baada ya kusomewa maelezo hayo na upande wa mashtaka, Mhindi alikiri kutenda kosa na mahakama kumpa adhabu hiyo au kifungo cha miezi sita gerezani.

Hakimu Katemana aliieleza Mahakama hiyo kuwa baada ya mshtakiwa kukiri maelezo yote ya kosa,inamtia hatiani na kumsomea hukumu pamoja na adhabu.

Akisoma hukumu hiyo,alisema amezingatia maelezo ya upande wa mashtaka na maelezo ya mshtakiwa alipokuwa akiililia mahakama na hivyo kumpa adhabu ya kulipa faini ya Sh.1000 au kwenda gerezani miezi sita.