Thursday, November 28, 2013

ZITTO KABWE APONZWA NA WALAKA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Chadema kimesema kwamba kilifikia uamuzi wa kumvua nyadhifa zake, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wake, Zitto Kabwe kutokana na sababu moja tu ya kuhusika katika Waraka wa Mkakati wa Mabadiliko 2013.

TANZANIA, BURUNDI DRC ZAUNDA UMOJA



Wakati Kenya, Rwanda na Uganda zimeunda umoja unaoitwa `Umoja wa Walio Tayari’ , Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) nazo zimeanzisha ushirikiano baina yao. Katika siku za karibuni kumekuwa na mtikisiko ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) baada ya Tanzania na Burundi kutengwa na wenzao wa Kenya, Rwanda na Uganda katika baadhi ya masuala muhimu ya ushirikiano hasa wa kiuchumi.

Tanzania, Burundi na DRC nazo zimekutana ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambaye aliliambia Bunge lililopita kuwa Tanzania inafikiria kushirikiana na nchi hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa Ujirani Mwema uliofanyika mjini Bujumbura, Burundi jana, Sitta alisema Tanzania, Burundi na Kongo zimekubaliana kuendeleza miundombinu ya barabara, reli, anga na usafiri wa maji katika Ziwa Tanganyika.

Sunday, November 24, 2013

TAARIFA YA ZITTO ZUBERI KABWE (MB) KUHUSU KUVULIWA NAFASI ZA UONGOZI NDANI YA CHAMA CHANGU CHA CHADEMA

1. Utangulizi

i. Katika kikao chake cha siku mbili kilichofanyika tarehe 20 ­ 22 Novemba 2013, Kamati Kuu ya CHADEMA, pamoja na mambo mengine, iliazimia kunivua nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama. Kwa mujibu wa taarifa ya chama iliyotolewa katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, ilielezwa kwamba sababu za kuvuliwa uongozi mimi na Dk Kitila Mkumbo ni uhaini na hujuma kwa chama kutokana na waraka unaojulikana kama mkakati wa uchaguzi 2013. Ukweli ni kwamba waraka uliotajwa si sababu ya mimi kuvuliwa nafasi zangu za uongozi kama ilivyojadiliwa katika Kikao cha Kamati Kuu . Sababu za kufukuzwa kwangu kama zilizojadiliwa katika kikao cha Kamati Kuu ni tuhuma lukuki ambazo si mara yangu ya kwanza kuzisikia zikijadiliwa ndani na nje ya vikao vya chama. Hitimisho la tuhuma hizi ni kwamba mimi nimekuwa nikikisaliti chama kwa kutumika na CCM na Usalama wa Taifa.

Nitazianisha tuhuma hizi na kuzijibu kama ambavyo nimekuwa nikizijibu katika vikao mbalimbali vyama.

ii. Ninatambua kwamba chama changu kinapita katika wakati mgumu sana sasa hivi. Nataka nitamke mapema sana kwamba

ZITTO KABWE AIGOMEA KAMATI KUU


MBUNGE wa Chadema ambaye pia ni Naibu kiongozi wa kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe amefunguka na kusema hayupo tayari kuondoka katika chama hicho hadi watakapoanza wao kuondoka.

Zitto ameyazungumza hayo leo jioni katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam alipokuwa anazungumzia maamuzi yaliyotolewa na kamati ya chama hicho kumvua nafasi zake zote za uongozi yeye pamoja na Mjumbe wa Kamati kuu ya chma hicho Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Arusha Samson Mwigamba.

Zito amedai hakuhusika wala kujua waraka wa siri ambao ndio uliosabababisha kumvua madaraka baada ya uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho kuunasa waraka huo.

Tuesday, November 19, 2013

WABUNGE EALA MATATIZO NCHI ZA MAZIWA KUPATA SULUHISHO


WABUNGE wanaoiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki wamesema suluhisho la matatizo ya nchi za Maziwa Makuu yatapata ufumbuzi wa kudumu iwapo kutakuwa na utaratibu wa kukaa meza moja kwa pande zote husika na kufanya mazungumzo ya kuleta amani.

Hayo yalisemwa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa wabunge hao, Adam Kimbisa wakati akizungumza na waandishi

wa habari jijini Dar es salaam ambapo pia alipongeza hotuba ya Rais Jakaya Kikwete alioitoa Bungeni Dodoma Novemba 7 mwaka huu juu ya Jumuiya hiyo.

“Sisi tunaamini amani ni jambo la msingi katika Afrika Mashariki na hasa katika nchi zilizo katika Maziwa Makuu. Tunawapongeza wanajeshi wetu na wanajeshi Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri walioifanya iliyowezesha mafanikio kupatikana” alisema.

Akielezea juu ya baadhi ya nchi wanachama wa EAC ambao ndio waanzilishi wa vurugu mbalimbali na migogoro Mwenyekiti huyo alisema kuwa Tanzania imekomaa kisiasa hivyo hawawezi kuwaondoa wale wanaoleta chokochoko kwa kuwa dawa ni kuzungumza na sio kuwatoa.

Mtangamano

Aidha Kimbisa amesema misingi ya Utengamano wa kiuchumi ikijengeka vizuri na kufanya kazi ipasavyo wananchi wote wa Afrika Mashariki watafaidika na hivyo suala la kuruka hatua yoyote ni jambo lisilokubalika.

“Tunaungana na kauli ya Rais kwamba Tanzania ni kati ya nchi zinazotaka ngazi zote za mchakato wa Mtangamano zitekelezwe moja baada ya nyingine bila kuruka hatua yoyote. Hatua ya kwanza ni Umoja wa Forodha inafuata soko la Pamoja kasha Umoja wa Fedha na hatimaye shirikisho la Kisiasa” alisema.

Alisema hadi sasa ni hatua mbili zilizotiwa saini na mchakato wa kuweka saini Umoja wa fedha unatarajiwa kutiwa saini baada ya kikao cha Juu cha Marais kinachotarajiwa kufanyika mjini Kampala Novemba 30 iwapo masuala yote muhimu ya mchakato huo yatakuwa yamekamilika.

“Jambo la msingi ambalo hata Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya imesema wazi kwamba Jumuiya lazima iwe ni ya wananchi kwa manufaa ya wananchi na isiwe ya viongozi. Wananchi washirikishwe katika kila hatua na kila ngazi ili iweze kushiriki kikamilifu kwa ajili ya maslahi yao” alisema.

Kuhusu VISA alisema kuwa wao wanaruhusu nchi nyingine kuendelea lakini Tanzania bado hawajafikia muafaka kwa kuwa wanaangalia maslahi ya nchi kwanza. Katika Hatua nyingine, Wabunge hao walimpongeza Rais Kikwete kupeleka kikosi cha Wanajeshi katika Brigedia Maalum iliyoundwa na Umoja wa Mataifa ili kuongeza nguvu ya kudhibiti waasi Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Thursday, November 14, 2013

WATAKAOVUJISHA TAALIFA ZA SIMU KUKAMATWA

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kampuni za simu za mikononi, zimewataka wateja watakaokumbwa na tatizo la kuvujishwa kwa taarifa za simu, kuripoti kwenye vyombo vya dola ili hatua zichukuliwe.

Aidha imeelezwa kuwa ingawa kumekuwa na mashine za kuzuia taarifa za siri za simu za mikononi kutovuja, baadhi ya wafanyakazi wa kampuni za simu wasio waaminifu wamekuwa wakihujumu wateja kinyume cha sheria kwa kuchezea teknolojia isivyopaswa.

Hadhari hiyo imekuja kukiwa na wimbi la matumizi mabaya ya simu za mkononi nchini, ikiwemo matumizi ya teknolojia kutoa hadharani mawasiliano ya siri ya watu.

Miongoni mwa matukio ya hivi karibuni, ni taarifa zilizoanikwa kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Kabwe Zitto, zikionesha mawasiliano ya siri anayodaiwa kufanya na watu mbalimbali yakidaiwa kuwa ni ya kuhujumu chama chake.

Tuesday, November 12, 2013

MKUU WA SHULE ABAMBWA AKIVUJISHA MAJIBU YA MTIHANI

MKUU wa Shule ya Sekondari ya Nkinto wilaya ya Mkalama, Monica Sebastian (30) na mwalimu wa kawaida wa shule hiyo, Agaloslo Otieno (32), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kuvujisha matihani wa kidato cha nne unaoendelea kufanyika hivi sasa nchini kote.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo lilitokea juzi, saa tatu usiku, katika shule hiyo kata ya Mwangeza tarafa ya Kirumi wilayani humo.

Alisema kuwa Mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani katika Shule ya Sekondari Mwangeza, alikuwa anaandika baadhi ya maswali ya Kiswahili na Civics kwenye simu yake ya kingajani na kumtumia Mwalimu Monica, akiwa shuleni kwake Nkinto.

Kamwela alisema baada ya Monica kupata maswali hayo, alikuwa anayatafutia majibu akiwa chooni na wanafunzi walikuwa wanamfuata huko huko chooni ili awapatie majibu hayo.

"Lengo lao ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao wa kidato cha nne mwaka huu. Wanafunzi waliambiwa kuwa wawe wanadanganya kwamba wanaenda kujisadia chooni ili wakapatiwe majibu na mkuu wa shule," alisema kamanda huyo na kuongeza; "Uchunguzi wa awali wa polisi unaonyesha kuwa, uvunjishaji huo ulifanyika kwa nyakati tofauti kati ya Mkuu wa Shule Monica na Mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani huo katika shule nyingine.
“Baada ya Mwalimu Monica kutumiwa maswali alikuwa anajificha chooni na wanafunzi kwa nyakati tofauti huomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda chooni kwa nia ya kujisaidia, ambapo humkuta mwalimu huyo na kuwapa maelekezo ya namna ya kujibu maswali hayo," alisema.

Alisema baada ya polisi kupata taarifa ya siri kutoka kwa wasamaria wema, waliweka mtego shuleni Nkinto na kufanikiwa kumkamata Mwalimu Monica, huku simu yake ikiwa na baadhi ya maswali ya mtihani.

Alisema polisi inaendelea na upelelezi zaidi, na kwamba mara utakapomalizika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili.

Friday, November 8, 2013

HOTUBA YA RAIS KIKWETE JANA

Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.
Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia “Operesheni Tokomeza”. Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.

Wednesday, November 6, 2013

MFANYAKAZI TBC AUWAWA

Mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji Nchini TBC, pichani,RAMADHAN GIZE ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosaidiwa kuwa ni majambazi usiku wa kuamkia leo katika eneo la UBUNGO Maziwa Jijini DSM.


Tukio hilo limetokea baada ya watu hao kuvamia duka moja katika eneo hilo la UBUNGO MAZIWA kwa lengo la kupora, ambapo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la MWARAMI RAJABU amejeruhiwa kwa kupigwa risasi na watu hao wanaosaidiwa kuwa majambazi.