Sunday, November 24, 2013

ZITTO KABWE AIGOMEA KAMATI KUU


MBUNGE wa Chadema ambaye pia ni Naibu kiongozi wa kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe amefunguka na kusema hayupo tayari kuondoka katika chama hicho hadi watakapoanza wao kuondoka.

Zitto ameyazungumza hayo leo jioni katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam alipokuwa anazungumzia maamuzi yaliyotolewa na kamati ya chama hicho kumvua nafasi zake zote za uongozi yeye pamoja na Mjumbe wa Kamati kuu ya chma hicho Dk. Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Arusha Samson Mwigamba.

Zito amedai hakuhusika wala kujua waraka wa siri ambao ndio uliosabababisha kumvua madaraka baada ya uamuzi wa Kamati Kuu ya chama hicho kuunasa waraka huo.

No comments:

Post a Comment